Na Mwamvua Mwinyi,Rufiji April 23


Patrick Golwike (Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Wenye Mahitaji Maalum [WMJJWM]) ameridhishwa na misaada inayoelekezwa na huduma zinazoelekezwa kwa akinamama waliojifungua na watoto waliokumbwa na maafa ya mafuriko Rufiji na Kibiti mkoani Pwani.

Aidha amepongeza mkoa,maofisa ustawi wa jamii kata,wilaya na mkoa kwa namna wanavyosimamia  makundi ya Wanawake waliojifungua, wenye watoto na vijana wa kike ambao wapo kwenye ukuaji.

"Nichukue fursa hii pia kuwapongeza watalaam wa Maendeleo ya Jamii wakiongozwa na Afisa Maendeleo ya Jamii mkoa wa Pwani ambae ni mratibu wa Maafa Mkoa wa Pwani Roseline Kimaro ,ambao wamekuwa wakitekeleza jukumu la uratibu  wa kuhakikisha waathirika wa mafuriko katika kambi Tano zilizopo kibiti na Ruiji wanapata huduma za msingi hasa wanawake ,watoto,wazee,na wenye  mahitaji maalumu."alifafanua.

Hata hivyo kuhakikisha huduma za msingi zinatolewa kwa makundi hayo, mabinti balee kujilinda ,ulinzi wa watoto na kutoa elimu ya lishe na saikolojia  .

Nae Mratibu wa maafa Roseline Kimaro alifarijika kuona wadau ambao wanapeleka misaada muhimu hasa kwa akinamama waliojifungua , watoto na mabinti balee.

"Ninawashukuru na umoja wa wanawake Tanzania, na mkoa kwa kujitoa kwao kupeleka mahitaji muhimu ya wanawake ikiwemo pedi,pempas,mabeseni,,nguo ,vyombo na vyakula kwani ni kama walijua kwamba ni moja ya changamoto ambazo ziliainishwa kuwakabili wanawake na watoto "alibainisha Roseline.

Roseline aliomba wadau wa jamii kuendelea kuwakimbilia kundi la wanawake, watoto,vijana na akinamama wajawazito na waliojifungua ili kuwapunguzia changamoto zinazowakabili.


 

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Wazazi Tanzania Jumuiya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndg.Ally Salum Hapi (MNEC) ametembelea na kuona treni mpya ya kisasa ya mwendokasi iliyowasili, Jijini Dodoma jana usiku ikitokea Jijini Dar Es Salaam iliyokuja na viongozi mbalimbali wa dini na serikali, wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Ndg.Masanja Kadogosa, pamoja na waandishi kwa ajili ya kuahiriki Dua Maalumu ya Kuliombea Taifa iliyofanyika katika Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, leo, ambapo Mgeni Rasmi Alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.Phillip Isdor Mpango.

Akizungumza baada ya kutembelea na kuona ubora, uzuri na utendaji kazi wa treni hiyo, Katibu Mkuu Wazazi, Ndg.Hapi, aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, kwa kutekeleza Ilani ya CCM ya Mwaka 2020 - 2024 kwa vitendo na kusema anastahili kuongezewa hali, morali na moyo wa kuendelea kuwatumikia wananchi wa Tanzania.

"Kwa niaba ya viongozi, wanachama na wapenzi wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM nichukue fursa hii adhimu kumpongeza Mwenyekiti wa CCM na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, kwa kuhakikisha mradi wa ujenzi wa reli ya mwendokasi kutoka Dar Es Salaam hadi Dodoma imekamilika kwa asilimia kubwa pamoja na majaribio ya treni ya mwendokasi na mabehewa yake kuletwa nchini na kuanza kufanyia majaribio yanayotoa matokeo chanya;

"Ama kwa hakika hii ni furaha na faraja kubwa sana kwetu sisi wamiliki wa duka kuona muuza duka wetu anaiendesha vizuri biashara yetu na matokeo chanya yanaonekana, lakini pia nitoe pongezi kwa watumishi wote wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) kwa usimamizi bora wa fedha za mradi huu ambao ni Tshs.Bilioni 23.5 ni fedha nyingi mnoo ila ndugu zetu hawa wanastahili pongezi kwa kusimamia vyema fedha hizo" alisema Hapi.

Akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi wa TRC, Ndg.Masanja Kadogosa, alitoa shukurani kwa viongozi na wanachama wa Jumuiya ya Wazazi kwa kutembelea mradi huo kwa kusema kwao watumishi wa Shirika la Reli Tanzania hujisikia ufahari wa hali ya juu inapotokea nafasi ya viongozi wa CCM na Jumuiya zake wanapotembelea mradi wa ujenzi wa reli ya mwendokasi na kusifia kwa kile kilichofanyika inawatia moyo na morali wa kuendelea kutumikia shirika na serikali kwa maslahi mapana ya nchi.

Katika msafara wake Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi, Ndg.Hapi, aliongozana na Naibu Katibu Mkuu Wazazi Bara, Ndg.Joshua Mirumbe Chacha, viongozi wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dodoma, Wilaya pamoja na kata husika kwa kujitoa kuungana nao kutembelea na kutazama mradi huo.






MFANYABIASHARA Marik Ngutti wa Machimbo ya Matabi wilayani Chato Mkoa wa Geita ameeleza namna ambavyo ufuatiliaji wake wa elimu ya mlipa kodi ilivyomnasua kutoka kwenye mikono ya matapeli waliojifanya maofisa Mamlaka ya Mapato (TRA).

Ngutti ametoa ushuhuda huo leo Aprili 23, 2024 alipotembelea banda la TRA katika maonesho ya Wakandarasi Geita Mjini kwenye viwanja vya EPZ ambapo amesema aliwapa elimu na wafanya biashara wenzake ambao pia walishindwa kutapeliwa baada ya kupata taarifa muhimu kuhusu maofisa wa TRA.

"Kuna watu walikuja kwenye maeneo yetu ya biashara pale Machimbo ya Matabi walijitambulisha kuwa ni maofisa wa TRA niliwajengea mashaka kwa kuwa niliona hawana utambulisho wa TRA na hawakuwa wanatoa lisiti kwa wenzetu waliotangulia kupita nikawaambia wafanyabiashara wenzangu kuwa hao sio maofisa wa TRA nikawapa namba ya TRA"

Amesema kwa kuwa tayari alishawapa elimu ya mlipa kodi walivyofika wale maofisa bandia wa TRA wale wafanyabiashara waliwahoji mambo muhimu yanayohusu TRA waliposhindwa kujibu wakaondoka zao na .

Ngutti amesema kuwa ufahamu juu ya masuala muhimu ya kodi na maofisa wa TRA ameyapata kutokana na jitihada zake za kufuatilia vipindi mbalimbali vya runinga na radio na kuwasisitiza wananchi wote kujielimisha katika masula muhimu ya kodi.




Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze ,Ridhiwani Kikwete amewataka wanafunzi na vijana kuacha matumizi mabaya ya mitandao, mambo yaliyo nje ya tamaduni za kitanzania na badala Yake watumie mitandao hiyo kujifunza na kujipa uelewa zaidi katika masuala ya masomo na elimu.

Aidha amewaasa kusoma kwa bidii kwani elimu ndio nguzo ya maisha yao.

Ridhiwani alitoa rai hiyo alipokuwa akihutubia wahutimu wa kidato cha sita shule ya sekondari ya Lugoba , Halmashauri ya Chalinze, mkoani Pwani.

Aliwaasa wahitimu hao kuhakikisha wanafaulu ili waache deni la kufuatwa na wadogo zao wanaowafuata kwa upande mmoja, wawape heshima walimu na wazazi kwa kufaulu vizuri.

Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ,Abdallah Sakasa aliishukuru serikali kwa kuendelea kupeleka pesa za elimu bure , vifaa na kuongezeka kwa madarasa na walimu shuleni hapo .

Alimuomba mbunge kuendelea kuikumbuka shule hiyo kwa kuisaidia vifaa na kuongeza mabweni ya wanafunzi.









MAHAKAMA ya Rufani leo imeshindwa kuendelea na usikilizwaji wa shauri la rufaa lililokatwa na Benki ya Equity Bank Tanzania Limited na Equity Bank Kenya Limited dhidi ya kampuni ya mafuta ya State Oil, kutokana na kesi ya msingi kusikilizwa bila hati ya madai kufanyiwa marekebisho.

Benki zilikata rufaa hiyo kupinga hukumu ya Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara iliyoipa ushindi kampuni ya State Oil inayodaiwa kukataa kulipa mkopo iliyopewa na benki hizo wa USD 18,640,000.

Rufaa hiyo ilikuwa imepangwa kusikilizwa leo tarehe 23, 2024 mbele ya jopo la majaji Rehema Mkuye, Abraham Mwampash na Zainabu Muruke.

Lakini majaji hao kabla ya kuanza kusikiliza rufaa hiyo wakawahoji mawakili kama ni sawa kesi ya msingi kusikilizwa bila hati ya madai kufanyiwa marekebisho baada ya Equity benki ya Kenya kujiunga katika kesi hiyo.

Mawakili wanaoziwakilisha benki hizo, Mpaya Kamala na Timon Vitalis wameieleza mahakama kuwa japo kweli kanuni zinasema kuwa baada ya kuongezwa mdaiwa mwingine hati ya madai ilipaswa kufanyiwa marekebisho, lakini wao hawaoni kama kutokufanya marekebisho ni tatizo kwani kutokufanya hivyo hakukuathiri upande wowote.

Mawakili hao kwa nyakati tofauti wamesema kuwa hata hivyo amri ya 1, Kanuni ya 10 (4) za Mwenendo wa Mashauri ya Madai (CPC) inampa jaji uhuru wa kuamua vinginevyo badala ya kuamuru hati ya madai kufanyiwa marekebisho na kwamba ndivyo jaji aliyesikiliza kesi hiyo ya msingi alivyoamuru.

“Hapa baada ya mdaiwa wa pili, Equity Kenya kuunganishwa jaji aliamuru kuwa wadaiwa wawasilishe maelezo yao ya utetezi wa maandishi. Na sisi tunaona hakukuwa na tatizo kwani hakukuathiri upande wowote”, amesema wakili Kamara.

Wakili wa kampuni ya State Oili Frank Mwalongo naye amesema kuwa anakubaliana na hoja za mawakili wenzake kuwa haikuwa muhimu kufanya marekebisho ya hati ya madai kwa kuwa kutokufanya hivyo hakujaathiri upande wowote.

“Kwa hiyo naiomba mahakama ione kwamba hoja hii haikuathiri upande wowote na Jaji alitenda kwa mujibu wa sheria na tuendelee na usikilizwaji wa rufaa.”

Baada ya mawakili hao kumaliza kutoa hoja zao kuhusu suala hilo, Jaji Mkuye ameahirisha kesi hiyo akisema kuwa mahakama itawajulisha pande zote siku ya kutoa uamuzi utakapokuwa tayari.

Kampuni ya State Oil inadaiwa kuwa ilidhaminiwa na Benki ya Equity Kenya kuchukua mkopo wa USD 18,640,000 kutoka kwa kampuni Lamar Commodity Trading DMMC ya Dubai, huku na yenyewe ikiikabidhi Benki ya Equity ya Kenya hati za mali zake mbalimbali kama dhamana ya udhamini wa mkopo huo.

Indaiwa kuwa hata hivyo haikuweza kulipa mkopo huo, hivyo Benki ya Equity Tanzania kama mdhamini wake ndio ikalipa mkopo huo kwa kampuni ya Lamar Commodity.

Benki ya Equity Kenya baada ya kuanza kuidai kampuni hiyo mkopo huo kupitia kwa Benki ya Equity Tanzania, ambayo ndio iliyopewa jukumu la kusimamia dhamana zilizowekwa na State Oil, kampuni hiyo ilikimbilia mahakamani ambako iliifungulia kesi Benki ya Equity Tanzania ikipinga kudaiwa mkopo huo.

Kabla ya kesi hiyo kuanza kusikilizwa Benki ya Equity Tanzania iliwasilisha maombi mahakamani hapo ili Benki ya Equity Kenya nayo ijumuishwe kwenye kesi hiyo na Jaji aliyeisikiliza akaikubalia akaamuru Benki ya Equity Kenya nayo ikaunganishwa kwenye kesi hiyo.

Benki hiyo ya Kenya ilipounganishwa mahakama haikutoa amri ya kufanya marekebishoa ya hati ya madai badala yake iliamuru tu benki hizo ambazo zilikuwa wadaiwa katika kesi hiyo ziwasilishe utetezi wake wa maandishi, kisha ikaendelea na usikilizwaji mpaka ikatoa hukumu.

Katika kesi hiyo kampuni hiyo iliiomba mahakama itamke kuwa ilishalipa mkopo wake wote iliokuwa inadaiwa na kwamba haina benki hizo hazina madai yoyote dhidi yake na pia ikaomba mahakama iamuru irejeshewe hati za mali zake ilizokuwa imezitoa kama dhamana ya kupata udhamini wa mkopo huo.

Benki katika utetezi wake ziliita mashahidi sita akiwemo na mwakilishi wa kampuni ya Lamar aliyetoa ushahidi jinsi alivyoikopesha State Oil fedha hizo kwa kudhaminiwa na Benki ya Equity na kwamba ilishindwa kurejesha mkopo huo na ikabidi benki hiyo iliyomdhamini ndio ikalipa mkopo huo.

Mahakama hiyo katika hukumu yake iliyotolewa Oktoba Mosi, 2021, ilikubaliana na madai na ushahidi wa State Oil kupitia kwa shahidi wake mmoja, kuwa ilikuwa imeshalipa deni lake lote na hivyo benki hizo hazikuwa na madai dhidi yake na ikaamuru State Oil irejeshewe hati zake za mali ilizoweka dhamana.

WATU  watatu wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani Pwani wakikabiliwa na mashtaka ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya Methemphetamine zenye uzito wa Kilogramu 424.84 pamoja na Heroin Hydrochloride gramu 158.24

Katika hati ya mashtaka iliyosomwa mahakamani hapo na wakili wa serikali Agness Ndanzi imewataja washtakiwa hao kuwa ni Rajabu Kisambwanda (42) mkazi wa Kerege Matumbi, Bakari Said (39) Mkazi wa Kunduchi Mtongani na Hillary Rhite (35) Mkazi wa Kunduchi Sodike.

Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda kosa hilo  kinyume na kifungu cha sheria cha  15 (1) (a) na cha (3) (i) cha Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Sura ya 95 kama illivyorejewa 2019. 

Wakisomewa mashtaka yao  mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Joyce Mkhoi  inadaiwa kuwa, Aprili 10, 2024 huko Zinga Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani, washtakiwa walikutwa wakisafirisha dawa hizo za kulevya 

Aidha Wakili Ndanzi alidai kuwa, siku na mahali hapo, mshtakiwa Bakari Said (39) Mkazi wa Kunduchi Mtongani alikutwa akisafirisha dawa za kulevya aina ya Heroin hydrochloride yenye uzito wa gramu 158.24.

Hata hivyo washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu kitu mahakamani hapo kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi ambazo kwa kawaida husikilizwa mahakama Kuu ama kwa kupewa kibali kutoka kwa DPP. 

Kwa mujibu wa upande wa Jamuhuri upelelezi katika kesi hiyo hado haujakamilika na kesi imeahirishwa hadi Mei, 7 2024 itakapokuja kwa ajili ya kutajwa.





 

Na Mwandishi wetu.

MAHAKAMA ya Rufani leo imeshindwa kuendelea na usikilizwaji wa shauri la rufaa lililokatwa na Benki ya Equity Bank Tanzania Limited na Equity Bank Kenya Limited  dhidi ya kampuni ya mafuta ya State Oil, kutokana na kesi ya msingi kusikilizwa bila hati ya madai kufanyiwa marekebisho.

Benki zilikata rufaa hiyo kupinga hukumu ya Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara iliyoipa ushindi kampuni ya State Oil inayodaiwa kukataa kulipa mkopo iliyopewa na benki hizo wa USD 18,640,000.

Rufaa hiyo ilikuwa imepangwa kusikilizwa leo tarehe 23, 2024 mbele ya jopo la majaji Rehema Mkuye, Abraham Mwampash na Zainabu Muruke.

Lakini majaji hao kabla ya kuanza kusikiliza rufaa hiyo wakawahoji mawakili kama ni sawa kesi ya msingi kusikilizwa bila hati ya madai kufanyiwa marekebisho baada ya Equity benki ya Kenya kujiunga katika kesi hiyo.

Mawakili wanaoziwakilisha benki hizo, Mpaya Kamala na Timon Vitalis wameieleza mahakama kuwa japo kweli kanuni zinasema kuwa baada ya kuongezwa mdaiwa mwingine hati ya madai ilipaswa kufanyiwa marekebisho, lakini wao hawaoni kama kutokufanya marekebisho ni tatizo kwani kutokufanya hivyo hakukuathiri upande wowote.

Mawakili hao kwa nyakati tofauti wamesema kuwa hata hivyo amri ya 1, Kanuni ya 10 (4) za Mwenendo wa Mashauri ya Madai (CPC) inampa jaji uhuru wa kuamua vinginevyo badala ya kuamuru hati ya madai kufanyiwa marekebisho na kwamba ndivyo jaji aliyesikiliza kesi hiyo ya msingi alivyoamuru.

“Hapa baada ya mdaiwa wa pili, Equity Kenya kuunganishwa jaji aliamuru kuwa wadaiwa wawasilishe maelezo yao ya utetezi wa maandishi. Na sisi tunaona hakukuwa na tatizo kwani hakukuathiri upande wowote”, amesema wakili Kamara.

Wakili wa kampuni ya State Oili Frank Mwalongo naye amesema kuwa anakubaliana na hoja za mawakili wenzake kuwa  haikuwa muhimu kufanya marekebisho ya hati ya madai kwa kuwa kutokufanya hivyo hakujaathiri upande wowote.

“Kwa hiyo naiomba mahakama ione kwamba hoja hii haikuathiri upande wowote na Jaji alitenda kwa mujibu wa sheria na tuendelee na usikilizwaji wa rufaa.”

Baada ya mawakili hao kumaliza kutoa hoja zao kuhusu suala hilo, Jaji Mkuye ameahirisha kesi hiyo akisema kuwa mahakama itawajulisha pande zote siku ya kutoa uamuzi utakapokuwa tayari.

Kampuni ya State Oil inadaiwa kuwa ilidhaminiwa na Benki ya Equity Kenya kuchukua mkopo wa USD 18,640,000 kutoka kwa kampuni Lamar Commodity Trading DMMC ya Dubai, huku na yenyewe ikiikabidhi Benki ya Equity ya Kenya  hati za mali zake mbalimbali kama dhamana ya udhamini wa mkopo huo.

Indaiwa kuwa hata hivyo haikuweza kulipa mkopo huo, hivyo Benki ya Equity Tanzania kama mdhamini wake ndio ikalipa mkopo huo kwa kampuni ya Lamar Commodity.

Benki ya Equity Kenya baada ya kuanza kuidai kampuni hiyo mkopo huo kupitia kwa Benki ya Equity Tanzania, ambayo ndio iliyopewa jukumu la kusimamia dhamana zilizowekwa na State Oil, kampuni hiyo ilikimbilia mahakamani ambako iliifungulia kesi Benki ya Equity Tanzania ikipinga kudaiwa mkopo huo.

Kabla ya kesi hiyo kuanza kusikilizwa Benki ya Equity Tanzania iliwasilisha maombi mahakamani hapo ili Benki ya Equity Kenya nayo ijumuishwe kwenye kesi hiyo na Jaji aliyeisikiliza akaikubalia akaamuru Benki ya Equity Kenya nayo ikaunganishwa kwenye kesi hiyo.

Benki hiyo ya Kenya ilipounganishwa mahakama haikutoa amri ya kufanya marekebishoa ya hati ya madai badala yake iliamuru tu benki hizo ambazo zilikuwa wadaiwa katika kesi hiyo ziwasilishe utetezi wake wa maandishi, kisha ikaendelea na usikilizwaji mpaka ikatoa hukumu.

Katika kesi hiyo kampuni hiyo iliiomba mahakama itamke kuwa ilishalipa mkopo wake wote iliokuwa inadaiwa na kwamba haina benki hizo hazina madai yoyote dhidi yake na pia ikaomba mahakama iamuru irejeshewe hati za mali zake ilizokuwa imezitoa kama dhamana ya kupata udhamini wa mkopo huo.

Benki katika utetezi wake ziliita mashahidi sita akiwemo na mwakilishi wa kampuni ya Lamar aliyetoa ushahidi jinsi alivyoikopesha State Oil fedha hizo kwa kudhaminiwa na Benki ya Equity na kwamba ilishindwa kurejesha mkopo huo na ikabidi benki hiyo iliyomdhamini ndio ikalipa mkopo huo.

Mahakama hiyo katika hukumu yake iliyotolewa Oktoba Mosi, 2021, ilikubaliana na madai na ushahidi wa  State Oil kupitia kwa shahidi wake mmoja, kuwa ilikuwa imeshalipa deni lake lote na hivyo benki hizo hazikuwa na madai dhidi yake na ikaamuru State Oil irejeshewe hati zake za mali ilizoweka dhamana.




 

Na Mwamvua Mwinyi, Kibaha April 24

Katibu wa CCM Wilaya Kibaha Mjini , mkoani Pwani, Issack Kalleiya amehimiza kuunda kamati za uchumi kila kata na matawi pamoja na kuanzisha vitenga uchumi ili kukiimarisha kiuchumi.

Wito huo aliutoa alipokuwa kata ya Kongowe ,ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kutembelea kata 14 ,yenye malengo wa kujitambulisha kukagua uhai wa Chama na Jumuiya na maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa.

Vilevile aliwaonya wanao wasumbua wenyeviti wa serikali za mitaa ,waache mara moja kwani kufanya hivyo ni kinyume na taribu za CCM ni kuvunja katiba na kanuni za maadili.

Kalleiya alielekeza viongozi wa CCM kuwaunga mkono na kufanya kazi na viongozi waliopo madarakani hadi watakapomaliza muda wao.

Alisisitiza kuongeza kasi ya hamasa kuongeza wanachama wapya kujisajili kielectronic na umuhimu wa kulipa ada ya uwanachama.

"Tuongeze nguvu, wanachama ni mtaji,hatunabudi kuendelea kushawishi ili kupata ongezeko kubwa la wanachama,licha ya wanachama tulipe ada ili kuwa hai,na tuelekeze kujiimarisha kwa kitu kimoja,tuungane,tuache makundi" alisisitiza Kalleiya.

Katibu Kalleiya pia amezungumza na watumishi wa serikali ngazi ya kata na mitaa kusikiliza maendeleo ya utekelezaji wa Ilani ya CCM chini ya Serikali ya dkt Samia Suluhu Hassan, Mbunge wa jimbo la Kibaha Mjini , Silvestry Koka na madiwani wote wa halmashauri Mji Kibaha na wenyeviti wa serikali za mitaa.
Na Mwamvua Mwinyi,RufijiApril 23

Patrick Golwike (Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Wenye Mahitaji Maalum [WMJJWM]) ameridhishwa na misaada inayoelekezwa na huduma zinazoelekezwa kwa akinamama waliojifungua na watoto waliokumbwa na maafa ya mafuriko Rufiji na Kibiti mkoani Pwani.

Aidha amepongeza mkoa,maofisa ustawi wa jamii kata,wilaya na mkoa kwa namna wanavyosimamia  makundi ya Wanawake waliojifungua, wenye watoto na vijana wa kike ambao wapo kwenye ukuaji.

"Nichukue fursa hii pia kuwapongeza watalaam wa Maendeleo ya Jamii wakiongozwa na Afisa Maendeleo ya Jamii mkoa wa Pwani ambae ni mratibu wa Maafa Mkoa wa Pwani Roseline Kimaro ,ambao wamekuwa wakitekeleza jukumu la uratibu  wa kuhakikisha waathirika wa mafuriko katika kambi Tano zilizopo kibiti na Ruiji wanapata huduma za msingi hasa wanawake ,watoto,wazee,na wenye  mahitaji maalumu."alifafanua.

Hata hivyo kuhakikisha huduma za msingi zinatolewa kwa makundi hayo, mabinti balee kujilinda ,ulinzi wa watoto na kutoa elimu ya lishe na saikolojia  .

Nae Mratibu wa maafa Roseline Kimaro alifarijika kuona wadau ambao wanapeleka misaada muhimu hasa kwa akinamama waliojifungua , watoto na mabinti balee.

"Ninawashukuru na umoja wa wanawake Tanzania, na mkoa kwa kujitoa kwao kupeleka mahitaji muhimu ya wanawake ikiwemo pedi,pempas,mabeseni,,nguo ,vyombo na vyakula kwani ni kama walijua kwamba ni moja ya changamoto ambazo ziliainishwa kuwakabili wanawake na watoto "alibainisha Roseline.

Roseline aliomba wadau wa jamii kuendelea kuwakimbilia kundi la wanawake, watoto,vijana na akinamama wajawazito na waliojifungua ili kuwapunguzia changamoto zinazowakabili.




 

 

Na: Calvin Gwabara – Mbeya.


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera kwa niaba ya Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amepongeza kazi nzuri ya Utafiti
iliyofanywa na SUA kwa kushirikiana na NEMC na kupelekea matokeo yake
kusambazwa kwenye nchi kumi zilizo ukanda wa magharibi mwa Bahari ya
Hindi.

Pongezi hizo zimetolewa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya
Mhe. Beno Malisa wakati akifunga mafunzo ya siku sita kwa Maafisa
Waandamizi wa Masula ya Maji na mazingira kutoka kwenye nchi nne
ikiwemo Madagaska,Msumbiji,Kenya na mwenyeji Tanzania ikiwa ni
sehemu ya kusambaza matokeo ya Mradi wa Utafiti wa Usimamizi
Endelevu wa Madakio ya Maji Kupitia Tathmini ya Kuimarisha Mtiririko
wa Maji kwa Mazingira na Utekelezaji wake katika Kulinda Ukanda wa
Magharibi mwa Bahari ya Hindi na Athari za Shughuli za Kibinadamu
Tanzania (EFLOWS).

“Kwa niaba ya Mkoa wa Mbeya nitumie nafasi hii kukipongeza Chuo Kikuu
cha Sokoine cha Kilimo kupitia kwa Mtafiti Mkuu wa Mradi huu wa
EFLOWS Prof. Japhet Kashaigili amabye ndiye mratibu wa mafunzo haya
kwa kazi nzuri waliyoifanya hadi sasa ambapo tunaona matokeo yake
yamewezesha nyinyi nyote kukutana nchini Tanzania ili kuona na kujifunza
matokeo mazuri kwa lengo la kwenda kuyatumia kwenye nchi zenu ili
kulinda mtiririko salama wa maji kuelekea baharini” alifafanua Mhe.Malisa
.
Amesema anaamini kuwa elimu waliyoipata kupitia Wataalamu wabobevu
kwenye masuala ya Tathimini ya maji kwa mazingira kutoka Tanzania na
Australia yatawawezesha kupata maarifa na mbinu ambazo zitasaidia wao
kutekeleza vyema mipango na kusimamia masuala ya usimamizi wa mito
na vyanzo vya maji kwa maslahi mapana na binadamu, Mazingira na
miradi mingine muhimu inayotegemea maji na ikolojia nzima.

Kwa upande wake Mtafiti Mkuu wa Mradi huo ambaye ni Mkurugenzi wa
Kurugenzi ya Uzamili, Utafiti, Uhawilishaji wa tekanolojia na Ushauri wa
kitaalamu kutoka SUA Prof. Japhet Kashaigili amesema utafiti huo ni moja
kati ya Miradi mitatu inayofadhiliwa na Programu ya WIOSAP nchini

Madagaska, Tanzania na Msumbiji katika kipindi cha miaka miwili na
nusu.

“Lengo la mradi huo ilikuwa ni kupunguza athari za shughuli za
kibinadamu ili kuimarisha Mtiririko wa Maji kwa Mazingira na Utekelezaji
wake katika Kulinda Ukanda wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi Kupitia
Tathmini ya Kuimarisha Mtiririko wa Maji kwa Mazingira na Utekelezaji
wake kwa ufadhili wa Mkataba wa Nairobi (Nairobi Convention) fedha
ambazo ni michango ya nchi wananchama ikiwemo Tanzania” alifafanua
Prof. kashaigili.

Aidha, Prof. Kashaigili amesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea
uwezo mameneja na Wataalamu kwenye nchi wananchama wa Ukanda wa
Magharibi mwa bahari ya Hindi kwenye masuala ya Tathimini ya maji kwa
mazingira na dhana ya “Kutoka kwenye chanzo hadi Baharini” (Source to
Sea) hasa katika kipindi hiki ambacho kuna changamoto kubwa za
uharibifu wa mazingira na vyanzo vya maji duniani.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo pia yatasaidia kujenga na kuzitazama
mbinu shirikishi ambazo zinaweza kutumika kusaidia kukabiliana na
changamoto ya athari za mtiririko wa maji kwa mazingira pamoja na
uchafuzi wa mazingira katika bahari na athari zake kwa viumbe maji.

Nae Wakili wa Serikali Mkuu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bwana
Wankyo Mnono amesisitiza umuhimu wa ushirikino kwa nchi zote zilizo
Magharibi mwa ukanda wa bahari ya Hindi kwakuwa ulinzi wake unahitaji
ushirikiano kwa nchi zote ili kufikia malengo ya mtiririko salama wa maji
kuelekea baharini pamoja na usalama wa bahari na viumbe maji wengine.

“Swala la ulinzi na usalama wa bahari ya Hindi linahitaji ushirikiano kwa
kila nchi katika kutelekeza makubaliano na kusimamia mtitiko wa maji
yake yanayoingia baharini, kukiwa na usimamizi kwenye nchi moja wakati
nchi nyingine ikifanya uharibifu changamoto hizi hazitaweza kumalizika
hivyo ni matumaini yangu kuwa baada ya mafunzo haya mmetengeneza
miongozo ambayo kila mmoja anakwenda kuhakikisha kwenye nchi yake
inatekelezeka” alisisitiza Wakili Wankyo.

Pamoja na mafunzo hayo pia washiriki wamepata nafasi ya kutembea
vyanzo vya maji na kuona jitihada zilizofanywa na mradi huo wa Utafiti wa
EFLOWS na Serikali kwenye eneo la Wanging’ombe Mkoani njombe na pia
kuzungumza na viongozi na Jumuiya za watumaia maji ikiwemo jumuiya ya
MBUMTILU.

Mradi wa Utafiti wa Usimamizi Endelevu wa Madakio ya Maji Kupitia
Tathmini ya Kuimarisha Mtiririko wa Maji kwa Mazingira na Utekelezaji
wake katika Kulinda Ukanda wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi na Athari
za Shughuli za Kibinadamu Tanzania (EFLOWS) unatekelezwa na Chuo
Kikuu cha Sokoine cha Kilimo kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la
hifadhi ya mazingira NEMC na wad au wengine kwa ufadhili wa
Sekretarieti ya Azimio la Nairobi.
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mhe. Beno Malisa wakati akifunga mafunzo kwa
niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera.
Mtafiti Mkuu wa Mradi huo ambaye ni Mkurugenzi wa Kurugenzi ya
Uzamili, Utafiti, Uhawilishaji wa tekanolojia na Ushauri wa kitaalamu kutoka
SUA Prof. Japhet Kashaigili akieleza malengo ya mafunzo hayo.
Wakili wa Serikali Mkuu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bwana Wankyo
Mnono akitoa salamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira.
Washiriki wa mafunzo hayo kutoka nchi nne za afrika wakiwa kwenye picha
ya pamoja na mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mhe. Beno Malisa
mara baada ya kufunga mafunzo hayo.
Washiriki wa mafunzo wakiangalia chanzo cha maji kwenye wilaya ya
Manging’ombe Mkoani Njombe wakiwa kwenye ziara ya mafunzo kuona
kazi zilizofanywa na mradi wa EFLOWS.
Washiriki wa mafunzo wakizungumza na Jumuiya ya watumia maji ya
MBUMTILU iliyopo Wilayani Wanging’ombe Mkoani Njombe kuona namna
jumuiya inavyoshiriki katika uhifadhi wa vyanzo vya maji.








WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso amesema Serikali inaendelea na maandalizi ya utekelezaji wa Gridi ya Taifa ya Maji inayolenga kutumia vyanzo vya uhakika vya maji ikiwemo maziwa na mito.

Ameyasema hayo leo April 23, 2024,jijini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa Buhigwe Kavejuru Felix aliyeuliza Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Mradi wa Grid ya Maji ya Taifa kwa kutoa maji Ziwa Victoria na Tanganyika.

Aweso amesema kwa sasa hatua iliyofikiwa ni ya kuajiri Mtaalam Mshauri atakayefanya upembuzi yakinifu wa mpango huo anatarajiwa kuajiriwa katika mwaka wa fedha 2024/25.

"Aidha,Serikali imeanza kutumia vyanzo vikubwa vya maji vya uhakika ikiwemo maziwa, mito mikubwa na mabwawa kwa ajili ya kusambaza huduma ya maji kwenye maeneo ambayo hayana vyanzo vya uhakika vya maji. Mfano ni mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria ambao umenufaisha Miji ya Kahama, Shinyanga, Tinde, Nzega, Tabora, Igunga na Shelui."amesema Aweso


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Ali Possi akiwasilisha hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la TCAA linalofanyika Morogoro
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la TCAA wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Ali Possi akiwasilisha hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo

Watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), wamepongezwa kwa kuendelea kufanya Baraza la Wafanyakazi lenye tija na kuhimizwa kuendelea kuwajibika ili kuwa chachu ya maamuzi makubwa ya kuboresha uboreshwaji wa huduma za Usafiri wa Anga nchini.

Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Ali Possi wakati wa ufunguzi wa Baraza la wafanyakazi la TCAA uliofanyika Aprili 23,2024 mjini Morogoro.

Pia ameongeza kuwa, kufanyika kwa vikao hivyo vya Baraza ni kuimarisha demokrasia mahala pa kazi,na kuwataka wajumbe wa Baraza hilo kurudisha mrejesho kwa watumishi wenzao ambapo pia amewahimiza watumishi wa TCAA kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuendelea kutenda kazi kwa ufanisi.

"Tunatambua umuhimu wa TCAA katika maendeleo ya nchi yetu lakini TCAA inajengwa kuianzia na wewe mtumishi mmoja, nawasihi sana mfanye kazi kwa kushirikiana kila mmoja kwa nafasi yake na inapobidi msaidie mwingine ili kuhakikisha malengo ya taasisi na serikali kwa ujumla yanafikiwa na huduma inatolewa" amesema Dkt. Possi.

Awali akizungumza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Bw. Daniel Malanga amesema Mamlaka inatekeleza Mradi wa ufungwaji wa mitambo ya Mfumo wa Mawasiliano kwa njia ya Sauti kati ya Rubani na Mwongoza ndege yaani VHF Radio Communication Systems ili kuboresha huduma ya Uongozaji Ndege katika Anga la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hii ikiwa na lengo la kuboresha mawasiliano katika anga la Tanzania.

“Mradi huu unatekelezwa kwa ufadhili wa Serikali kuu kwa fedha za kitanzania bilioni 31.5 ambapo Mamlaka iliandaa mahitaji yaani specification na kutangaza tenda shindanishi ambapo Kampuni ya Jotron AS ya Nchini Norway ilishinda zabuni na kuingia nayo mkataba na utakelezaji ulianza mara moja”

Mkurugenzi Malanga ameongeza kuwa,vingine ni kuendelea kutolewa kwa mafunzo kwa wataalam wa Usafiri wa Anga.

Na pia Bw. Malanga amezitaja baadhi ya changamoto hasa suala la upatikanaji na ucheleweshaji wa upatikanaji wa vibali vya ajira na upandaji wa madaraja kwa Watumishi wa TCAA. Kitendo ambacho kinashusha ari ya watumishi.

Baraza hilo linafanyika kwa siku mbili ambapo mbali na kujadili masuala kadhaa yanayoihusu TCAA wajumbe wamepata nafasi ya kupiga kura na kumchagua mfanyakazi bora wa Mamlaka kwa mwaka huu wa fedha.
Katibu wa Baraza Bw. Didacus Mweya (aliyesimama) akitoa salamu za utangulizi kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi kwa niaba ya wajumbe wa Baraza

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Bw. Daniel Malanga akiwasilisha hotuba ya Mkurugenzi Mkuu mbele ya Mgeni Rasmi pamoja na Wajumbe wa Baraza


Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la TCAA wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Bw. Daniel Malanga
Picha ya Pamoja


Top News